Sep 22, 2016

Posted by Dismas Ten Thursday, September 22, 2016 No comments


MCHEZO wa  ligi kuu ya soka Tanzania bara kati ya Mbeya City fc na Tanzania  Prison  uliochezwa kwenye uwanja wa Sokoine  jijini Mbeya  umemalizika kwa  suluhu ya bila  kufungana.

Kwenye mchezo huo uliokuwa wa vuta nikuvute, timu zote  zilishambuliana kwa zamu katika vipindi vyote viwili lakini hadi dakika 90 zinamalizika hakuna timu iliyofanikiwa  kuona lango la mwenzake.

Mabadiliko yaliyofanywa na kocha Kinnah Phiri kwa kuwatoa  Issa Nelson, Joseph Mahundi na Ramadhani  Chombo, na nafasi zao kuchukuliwa na Michael Kerenge, Ditram Nchimbi na Salvatory Nkulula hayakuweza kubadili matokeo ya mchezo huo uliozikutanisha timu hizi mbili hasimu.
Mara baada ya mchezo Kocha Phiri  pamoja na maneno mengine kadhaa  alisema kuwa makosa kadhaa kwenye safu ya ushambuliaji yaliinyima City ushindi kwenye mchezo huo.

“Timu imecheza vyema,tutafanyia kazi makosa kadhaa yaliyojitokeza leo kwenye safu yetu ya ushambuliaji, soka iko hivyo, ni jambo jema  tumepata pointi moja  tunaanza maandalizi ya mchezo ujao  tutakaocheza ugenini huko Mlandizi”, alisema.

0 COMMENTS:

TAFUTA HAPA

UNGANA NASI

Delicious Digg Facebook Favorites More Stumbleupon Twitter