Feb 15, 2012

Posted by Dismas Ten Wednesday, February 15, 2012 No comments
Siku chache baada ya kutolewa wa taarifa ya kutekezwa kwa timu ya Toto African ya jijini Mwanza inayoshiriki Ligi kuu ya Vodacoma Tanzania Bara, hatimaye kampuni ya uchimbaji madini Geita Gold Mine imeibuka na kuipatia timu hiyo kitita cha Shilingi Milioni 5 ili kuiongozea nguvu ya ushiriki wake katika ligi hiyo.

Katika makabidhiano hayo yaliyofanyika jana jijini humo mkuu wa mkoa huo Eng.Evarist Ndikilo aliutaka uongozi wa klabu hiyo kuutumia vizuri msaada huo ili usaidie katika kuiepusha timu hiyo na hatari ya kutelemka daraja hatimaye jiji hilo likakosa uwakilishi katika michuano ya Ligi kuu.

"Ni juzi tu tumetoka kusikio malalamiko ya ukata mkubwa uliokuwepo klabuni hapa, tunawashukuru GGM kwa msaada wao lakini nawaomba mtumie vizuri msaada huu ili tusije tukajikuta bado tunaendelea kubaki kwenye hatari ya kutelemka daraja na hatimaye Mwanza ikabaki kucheza mashindano ya ngazi za chini" alisema Ndikilo.

Katika hatua nyingine kampuni hiyo pia imetoa kiasi kama hicho kwa ajili ya kuisaidia timu maarufu ya Pamba Sc inayoshiriki ligi daraja la kwanza ili iweze kujipanga na hatimaye kurejea tena katika ligi kuu .


0 COMMENTS:

TAFUTA HAPA

UNGANA NASI

Delicious Digg Facebook Favorites More Stumbleupon Twitter