Mabeki wa Ruvu Shooting wakijaribu kumzuia Emmanuel Okwi wa Simba Afisa Habari wa Timu ya Soka ya Ruvu Shooting ya Mlandizi Kibaha Mkaoni Pwani Masau Bwire amejinasibu kuwa timu yake itaibuka na ushindi mnono katika mchezo wa Ligi Kuu ya Soka Tanzania Bara baina ya timu hizo unaotarajiwa kupigwa leo.
Akizungumza Asubuhi hii na SLT Bwire ambaye pia ni Afisa wa Habarai wa Chama cha soka mkoni humo ametamba kuwa licha ya uzuri wa timu hiyo kutoka mkoani Manyara lakini ana uhakika vijana wake wataibuka na ushindi kutokana na mipango mizuri iliyopo hivi sasa katika kikosi hicho.
"tunajua wana kikosi bora lakini nina hakika kuwa dakika tisini za mchezo wa leo sisi (Ruvu) tutaibuka na ushindi kutokanana mipango mizuri tuliyonayo hivi sasa" alisema Bwire










0 COMMENTS:
Post a Comment