Apr 28, 2012

Posted by Dismas Ten Saturday, April 28, 2012 No comments


Na Hemed Kisanda
Zikiwa  zimesalia siku chache kabla ya kupigwa kwa mchezo wa  watani wa jadi kwenye soka la  Bongo hapo Mei   mwaka  huu,  uchunguzi uliofanywa  na  blog hii  kutoka kwa  wadau mbalimbli wa  soka  umeonyesha kuipigia upatu Yanga  kuibuka na ushindi wa mabao 2-1 kwenye mcheo huo.
Wakizungumza kwa  nyakati tofauti kuhusu mechi hiyo inayotarajia  kupigwa kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar, mashabiki  wengi mamepiga kura ya kuipa  ushindi Yanga kwa madai kuwa  itaingia uwanjani  kwa kukamia  ikiwa na lengo la  kulinda heshima yake  hasa baada ya kuambulia patupu kwenye michuano ya ligi kuu  mwaka huu.
“Unajua ndugu yangu huu  ni msimu mbaya  kwa Yanga kwa kuwa  haina lolote la kujivunia,  naamini wataingia uwanjani kutka kurinda heshima na kuwapa faraja mashabiki wao , binafsi nahisi wanweza kupaa ushindi wa 2-1 dhidi ya  watani zao”  alisema  shabiki mmoja  aliyejitambulisha kwa jina la  Saddam na kudai kuwa  yeye ni shabiki wa kutupwa wa Ashanti  United.
Kaika hatua nyingine  shabiki mmoja wa Simba  ambaye hakupenda kutajwa  jina lake alisema  kuwa  ana hofu  timu yake itaingia uwanjani ikiwa imejiamini kupia kias jambo amabalo linaweza kuifanya Simba ikapoteza mchezo huo.
“Hakika timu yetu ni nzuri kwa sasa lakini wasiwasi  wangu ni kupoteza mchezo endapo wachezaji wataingia  uwanjani wakiwa  wamejiamini  kupita kiasi na  kuidharau Yanga  alisema shabiki huyo. 

0 COMMENTS:

TAFUTA HAPA

UNGANA NASI

Delicious Digg Facebook Favorites More Stumbleupon Twitter