May 3, 2012

Posted by Dismas Ten Thursday, May 03, 2012 No comments

Kiungo mahiri wa mabingwa wa soka msimu uliopita nchini, Yanga Haruna Niyonzima, amesema  hana mpango wa  kuondoka  katika  timu yake hiyo  kwa  wakati huu  ikiwa  ni  kulinda heshima  ya Rais  wa  nchi yake  Paul Kagame.


Akizungumza na SLT mapema mchana  huu  kutoka kwenye kambi ya  timu hiyo Wilayani Bagamoyo, Haruna  ambaye pia ni nahodha wa timu ya taifa ya Rwanda (Amavubi) amesema  kuwa  hafikirii  kuipa mkono wa kwaheri Yanga  kwa  kuwa kufanya hivyo atavunja  makubaliano aliyofanya na Rais  Kagame  wakati wa  usajiri wake kutoka  APR.


"Unajua wakati natoka APR kuja Yanga  nilitumia zaidi ya saa mbili kwenye ikulu ya  Rwanda nikizungumza na Rais juu  ya mimi kuicha timu yake kuja  Yanga, kimsingi tulizungumza mengi lakini  kikubwa  alichoniambia muheshimiwa  ni kuwa  kama itatokea  nimeshindwa  kuendelea  kuitumikia  Yanga  basi nimwambie  na mara moja atanitumia ndege kunirudisha  nyumbani  kwenye kikosi cha APR" alisema  HARUNA


Akiendelea zaidi  haruna alisema  kuwa  awali  aliwahi  kujaribu kwenda kucheza katika nchi kadhaa ulaya  kama  Ufaransa  Sweden  na Uturuki  lakini mara zote  rais Kagame  alikuwa  akimrudisha  kabla  ya kumaliza majaribio yake ili aisaidie  APR.

"MARA kadhaa nilijaribu kwenda Ulaya kucheza  lakini alikuwa akinirudisha kabla  sijamaliza majaribio kwa kuwa  alitaka niendelee kuichezea APR hivyo hata  kuja hapa  aliniruhusu kwa  shingo upande huku akinia  maagizo hayo na kubwa zaidi likiwa  ni kuwa hata yeye anaipenda YANGA"  alimaliza Haruna 

0 COMMENTS:

TAFUTA HAPA

UNGANA NASI

Delicious Digg Facebook Favorites More Stumbleupon Twitter