May 3, 2012

Posted by Dismas Ten Thursday, May 03, 2012 No comments

Na Hemed Kisanda


Msemaji wa  klabu ya  Simba  Ezekiel Kamwaga  (Mr Livepool) ametamba kuwa licha ya shirikisho la soka nchini  TFF kuusogeza mbele mchezo wa mwisho wa ligi  kuu ya soka Tanzania  Bara  dhidi  ya  watani zao Yanga  ana uhakika  kikosi chake  kitaibuka na ushindi mnono wa bao 3-0.


Akizungumza na   SLT mchana huu  kamwaga amesema  kuwa  tambo hizo zinatokana na  ushindi wa idadi hiyo  ya  mabao iliyoupata timu yake kwenye za hivi  karibuni  katika ligi hiyo na ule wa kombe la shirikisho  dhidi ya  Al Ahly  Shandy ya  Sudan.


"Najua vijana wataendeleas  rekodi yetu ulioyoiona katika mechi za hivi karibuni kwenye ligi na  pia  kwenye kombe la shirikisho kila timu  tuliyokutana nayo imekula  bao 3  na hata watani zetu  kipigo chao kitakuwa  ni hicho"alisema Kamwaga

0 COMMENTS:

TAFUTA HAPA

UNGANA NASI

Delicious Digg Facebook Favorites More Stumbleupon Twitter