Apr 24, 2012

Posted by Dismas Ten Tuesday, April 24, 2012 No comments


Nyota  wa  soka  Bongo,  Jerry son Tegete,  anayekipiga   kwenye  kikosi cha  mabingwa  wa zamani wa  soka  Tanzania Bara   Yanga , amesema   hana mpango wowote wa kuipa kisogo timu yake  katika kipindi kijacho cha  usajiri wa majira ya joto licha  ya  kuvurunda msimu huu.

Akizungumza na  blog  hii mapema leo Tegete ametanaibaisha kuwa  licha ya  timu yake  kukosa  Ubingwa  wa Ligi ya Tanzania Bara msimu huu bado  anataka kubaki kwenye kikosi hicho kwa  kuwa  anaimani  kubwa  kuwa uongozi wa timu hiyo utafanya  marekebisho  makubwa  na kuifanya Yanga kuwa  bora zaidi  msimu ujao.
“Ni wazi  kuwa  tumekosa ubingwa msimu huu, sina mawazo ya kuondoka Yanga, nataka  kubakia hapa, nina imani msimu ujao tutakuwa na kikosi bora  zaidi kuliko msimu huu,  hii  ni kwa sababu  najua uongozi utafanya marekebisho makubwa ikiwa ni pamoja na usajiri wa nguvu  katika kuuimarisha timu” alisema Tegete. 

0 COMMENTS:

TAFUTA HAPA

UNGANA NASI

Delicious Digg Facebook Favorites More Stumbleupon Twitter