May 8, 2012

Posted by Dismas Ten Tuesday, May 08, 2012 No comments

Siku chache  baada  ya  kupokea  kipigo cha  bao 5-0 kutoka  kwa  watani zao Simba  katika  mchezo wa  mwisho wa  ligi  kuu Tanzania  bara   uliopigwa  kwenye  uwanja  wa  Taifa  jumapili iliyopita  wadau na  mashabiki wa  Yanga  jijini mwanza  wameibuka  na kumtaka mwenyekiti wa  timu hiyo Lloyd  Nchunga  kujiuzuru.

wakizungumza  na blog hii  mapema  leo  mashabiki hao wamesema  kuwa  hakuna  utawala  mbovu uiliwahi kutokea  ndanai ya  klabu yao kama  huu  uiliopo  sasa  hivyo  mwenyekiti huyo ameshindwa  kuiongoza  klabu hiyo.

"Tunamtaka mwenyekiti ajiuzuru  kwani inatuuma  sana kufungwa  bao 5  na  watani zetu,  hakika  huu ni  uongozi mbovu kuwahi kutokea  katika  timu  yetu ,  tunamkumbuka  sana  mwenyekiti alieyepia  (Madega) licha ya  kuwa  alikuwa  na mapungufu  yake  lakini klabu haikuyumba  na kugawinyika  kama  ilivyo sasa"  walisema  Wadau  hao.

0 COMMENTS:

TAFUTA HAPA

UNGANA NASI

Delicious Digg Facebook Favorites More Stumbleupon Twitter