Jun 20, 2012

Posted by Dismas Ten Wednesday, June 20, 2012 No comments


Kamati ya usajili ya klabu yanga inayoongozwa na Salum Rupia kwa kushirikiana na kamati ya usajili sambamba na Benchi la ufundi la klabu hiyo, imejikuta katika wakati mgumu kufuatia wachezaji wake kadhaa wanaotakiwa kuondolewa katika orodha ya wachezaji wa klabu hiyo kwa ajili ya msimu ujao ligi kugomea hatua hiyo ya kuondoka ilhali bado wanamikataba ndabni ya klabu hiyo.
Kwa mujibu wa taarifa za ndani toka kwa mtu wa karibu na kamati hiyo ni mwamba mchezaji raia wa Ghana aliyesajiliwa na klabu hiyo kongwe barani mwaka 2010 kwa mbwembwe Kenneth Asamoah amegomea kukatishiwa mkataba wake kwa kile kilichoonekana kushindwa kuafikiana kwa baadhi ya mambo likiwemo suala zima la malipo ya kuukata mkataba huo ambao umesalia mwaka mmoja kumalizika.
Wachezaji wengine ambao nao wanatakiwa kupunguzwa na kupisha nafasi kwa wachezaji wengine ambao wanahitajika msimu huu ni Pamoja na Julias Mrope na Pius Kasambale ambao wote waliitwa na kamati ya usajili ya Yanga jana kuelezwa juu ya azma ya klabu hiyo kuwatafutia timu nyingine ambazo wataelekea huko kwa mkopo wameonekana kuchachamaa na kupinga hatua hiyo ya kamati ya usajili ya Yanga.
Hatua hiyo imezua utata na hali ya sintofahamu wakati huu ambapo shirikisho la soka nchini Tanzania TFF limetangaza kuongeza muda wa tarehe ya mwisho ya kutangaza wachezaji watakao achwa na vilabu mbalimbali huku  vigogo Simba na Yanga kama kawaida yao wakiendelea kusuasua kufanya hivyo.
Wakati dirisha la usajili likitarajiwa kufungwa tarehe 30/06/2012 Yanga tayari imesha kamilisha usajili wa wachezaji kadhaa akiwemo Kelvin Yondani toka Simba, Frank Domayo toka JKT Ruvu, Nizar Khalfani mchezaji huru aliyekuwa akichezea soka katika klabu Vancouver White Caps ya Canada na Ally Mustaafa  "Bartez" toka Simba.

0 COMMENTS:

TAFUTA HAPA

UNGANA NASI

Delicious Digg Facebook Favorites More Stumbleupon Twitter