Jun 11, 2012

Posted by Dismas Ten Monday, June 11, 2012 No comments

 MSHAMBULIAJI wa  Coastal Union ya Tanga , Ben Mwalala kuikacha  timu hiyo kuelekea  falme za  kiarabu  kucheza soka ya  kulipwa.

Akizungumza  na Blog hii  muda mfupi uliopita  Mwalala ametanabaisha kuwa atatimkia urabuni kujiunga  na klabu ya klabu ya Al- Teliya mara baada ya kumalizika kwa michuano ya Kombe la Kagame.

“Ni meambia  kuwa sitakuwa  katika kikosi cha Coastal  Union msimu ujao  hivyo nimeona ni bora kwenda  kusaka maisha mengine huko Uarabuni” alisema Mwalala.
Akiendelea zaidi  Mwalala aliyewahi kuitumia  Yanga ya  jijini Dar, aliarifu kuwa ni kawaida kwa mchezaji  kutokujumuishwa kwenye kikosi  kutokana na sababu mbalimbali ndiyo maana haja lalamika na amepanga kuelekeza nguvu zake  huko Uarabuni .

 “ Kabla ya kuja Coastal  nilikuwa  nacheza soka  kwenye klabu hiyo, ndiyo maana  imekuwa rahisi  kwangu kurudi kwa mara nyingine na ninatarajia kuondoka  hapa mara baada ya kumalizika michuano ijayo ya kombe la Kagame,” alisema Mwalala.

Mwalala ni miongoni mwa wachezaji tisa waliotemwa na Coastal Union katika  msimu ujao wa ligi kuu ya Bara sambamba na Ali Ahamed ‘Shiboli’.

0 COMMENTS:

TAFUTA HAPA

UNGANA NASI

Delicious Digg Facebook Favorites More Stumbleupon Twitter