Dec 23, 2010

Posted by Dismas Ten Thursday, December 23, 2010 1 comment
FLORA MVUNGI 'THE ONE'

Diva wa kiwanda cha filamu Bongo, Flora Mvungi amesema ameamua ‘kuipa kisogo’ kwa muda kambi hiyo na kujiunga na ‘gemu’ ya muziki wa kizazi kipya ‘Bongo Fleva’


Akisema na www.dismasten.blogspot.com ‘juzi kati’ ndani ya hotel ya Atriums pande za Sinza jijini Dar, nyota huyo wa filamu ya ‘Domestic Love’ alitanabaisha kuwa tangu kitambo alikuwa na ndoto ya kufanya muziki wa kizazi kipya lakini ratiba ndefu ya kazi za filamu imekuwa ikimnyima uhuru ndiyo maana sasa ameamua kuachana nayo na kugeukia Bongo Fleva.


“Unajua toka zamani nilikuwa na hamu ya kufanaya muziki lakini ratiba za filamu zilininyima uhuru ndiyo maana sasa nimeamua kuziweka kando, na hivi ninavyoongea na wewe tayari nimeshamamaliza kurekodi nwimbo wangu wa kwanza pale ‘Shalobaro Rec’ kwa Bob Junior” alisema Flora bila kutaja jina la wimbo huo

Posted by Dismas Ten in | Thursday, December 23, 2010 No comments
STEVEN CHARLES KANUMBA

I con wa kiwanda cha filamu Bongo, Steven Charles Kanumba ‘The Great’ amegoma kuyaanika hadharani mapato yanayopatika ktokanana uuzwaji wa filamu zinazotolewa na wasanii wanaondaa muvi nchini.

Akizungumza na www.dismasten.blogspot.com, mapema jana Kanumba aneyafanya vizuri sokoni na filamu yake ya ‘More Than Pain’ alisema licha ya kukua kwa tasnia ya filamu hapa nchini lakini suala la mapato yanayopatika baada ya filamu kuingizwa sokoni yanabaki kuwa siri ya mtayarishaji au watayarishaji wa filamu husika.

“Ni kweli kuwa tasnia ya filamu hivi sasa inakuwa hii ikiwa na maana kuwa wadau wetu, wameikubari na wananunua kazi zetu lakini suala la kiasi gani kinapatikana kwa mauzo ya filamu moja itabaki kuwa siri ya watayarishaji husika na kamwe siwezi kuisema hapa” alisema Kanumba.

Alipoulizwa kama uwoga huo wa kutaja mapato unatokana na kuogopa makali ya serikali Kanumba alisema hana uhakika juu ya hilo lakini anachokifahamu ni kuwa mapato bado yataendelea kubaki siri ya watayarishaji, mpaka hapo baadae hali itakapokuwa nzuri zaidi.

Sina hakika kama kuna mtu anawea kukwepa mkono wa serikali, lakini kwa sasa bado itaendelea kuwa hivyo mpaka hapo baadae mambo yatakapokuwa mazuri zaidi ndiyo tunaweza kutaja kiwango kinachopatikana alisema Kanumba.
Posted by Dismas Ten in | Thursday, December 23, 2010 No comments
SEIF SHAABAN 'MATONYA'

Nyota wa Muziki wa kizazi kipya Bongo, Seif Shaban ‘Matonya’ mwenye maskani yake pande za Tanga, ameibuka na kutupilia mbali tetesi kuwa ukimywa wake kwenye ‘gemu’ hivi sasa unatokana kuishiwa mashairi jambo linalomfanya kushindwa kutunga ngoma zenye kiwango kama alivyokuwa akifanya hapo awali.

Akizungumza na www.dismasten.blogspot , juzi kati pande za My fair jijini Dar Matonya aliyewahi kuitikisasa Bongo kwa ngoma ya ‘Vailetti’alifunguka kuwa kumekuwa na tetesi kitaa kuwa ameishiwa mashari na hawezi tena kufanya vizuri kwenye muziki kama alivyokuwa mwazo kwa kuwa sehemu kubwa ya nyimbo zilizokuwa zinampa chati wakati huo alikuwa akitungiwa na watu.

“Kaka mimi sijafulia kimawazo, bali ukimya wangu hivi sasa ni mikakati tu ya kujiweka sawa na mabadailliko ya muziki wetu unaoendelea kukua kila siku, kumbuka hivi sasa muziki ndiyo kila kitu kwenye maisha yangu kwa hiyo siwezi kufanya kazi kwa kukurupuka, nataka kufanya kazi kwa mpango na kusaka mafanikio kwenye levo za kimataifa zaidi” alisema Matonya ambaye pia ndiyo mtunzi wa kibao matata cha ‘Anita’.

Posted by Dismas Ten in | Thursday, December 23, 2010 No comments
ATHUMAN MWINGEREZA 'TANZANITE'

Nyota wa muziki wa kizazi kipya nchini Athumani Mwingereza ‘Tanzanite’ aliyeibukia mlango wa nyuma baada ya ‘kukopi na kupesti’ wimbo wa ‘Mbagala’ ulioimbwa na mkali Nasib Abdul ‘Diamond’ ameiacha kwenye mataa lebo iliyomtoa ya Matunguli Fleva na kutimkia Dhahabu Record inayoongozwa na ‘Handsome’ Abdul Abby Sykes ‘Dully Sykes’.

Akizungumza na www.dismasten.blogspot, Tanzanite alitanabaisha kuwa ameamua kuchukua hatua hiyo ikiwa ni mpango mmoja wapo wa kujiimarisha na kukuza kiwango chake cha muziki na pia kujiweka tayari kwa ujio wake mpya kwenye ‘gemu’ hiyo.

“Nimeamua kujiunga na Dhahabu Record ili kujiimarisha zaidi kimuziki huku pia lengo langu ikiwa ni kuweka sawa ujio wa kazi yangu mpya ambayo haitategemea mgongo wa mtu mwingine kama ambayo nilifanya kwenye wimbo wa ‘Kafara’” alisema Tanzanite

Posted by Dismas Ten in | Thursday, December 23, 2010 1 comment
STEVEN CHARLES KANUMBA
Msanii ‘matawi ya juu’ katika kiwanda cha filamu Bongo Steven Kanumba ‘The Great’ ameibuka na kukanusha vikali stori zilizoenea kitaa kuwa yeye na waaandaaji wengine wa filamu wakemuwa wakiwakimbilia mamiss, na kuwajumuisha kuigiza muvi kwa lengo la kuongeza kipato ilihali wakijua kwamba warembo hao hawana uwezo wa kuigiza.

Kanumba, ambaye hivi sasa anamiliki kampuni yake binafsi ya filamu inayokwenda kwa jina la Kanumba Film Production, alisema hayo wiki aliyopita katika mahojiano maalum na www.dismasten.blogspot.com, kufuatia kuwepo kwa malalamiko mengi ya wapenzi wa filamu juu ya kutumiwa kwa wasichana wenye umaarufu fulani wakati uwezo wao wa kuigiza ni mdogo.

“Ndiyo ni kweli tumesikia juu ya malalamiko, lakini mimi binafsi sijawahi kumuita wala kumtafuta miss ama msichana yoyote maarufu kwa ajili ya kazi isipokuwa wao ndiyo wamekuwa wakitupigia simu na kuomba tuwape kazi hiyo” alisema kanumba

Akiendelea zaidi msanii huyo ambaye kwa mara ya kwanza Muvi yake ya ‘Black Sunday’ imeonyeshwa kwenye majumba ya Sinema hapa nchini alianika kuwa kumekuwa na ugumu fulani katika kuwagundua wasanii wengine wenye vipaji ndiyo maana wamekuwa wakiamua kuwapa nafasi mamis wanaoomba kufanya kazi hiyo kwa kuwa wanapatikana kirahisi

“Nikiwa kama muandaaji wa filamu kuna sifa kama tano hivi ambazo mwigizaji anatakiwa awe nazo ili kupewa nafasi hiyo sasa inakuwa shida kidogo kwa wasichana wa mtaanii kuzikamilisha hii inatufanya kuwa na wakati mgumu sana wa kuwatafuta” alisema

Alipoulizwa aina ya sifa hizo Kanumba alizitaja kuwa ni pamoja na Uzuri wa sura, Umbo, kimo, elimu kwa maana ya kujua lugha tofauti, kutembea (Motion) na pia kujiamini.

Katika hatua nyingine nyota huyo anayesumbua sokoni na muvi yake ya ‘More than Pain’ aliwataka wasichana wanaoona kuwa wana uwezo na sifa za kuigiza, kukaa tayari kwani kuna mpango maalum ambao ameundaa kwa ajiri ya kutafuta vipaji vya wasichana kutoka mtaani

Posted by Dismas Ten in | Thursday, December 23, 2010 No comments
Zuwena Mohamed 'Shilole'
Nyota wanaofanya kweli katika kiwanda cha filamu Bongo, Zuena Mohamed ‘Shilole’ na Flora Mvungi ‘The One’ wanatarajia kukwea pipa mapema mwezi ujao kueleka Abuja nchini Nigeria kufuatia mwaliko wa kufanya filamu na dairekta maarufu wa muvi nchini humo Izu Ojukwu.


FLORA MVUNGI

Wakisema na gazeti hili, juzi kati, ndani ya mjengo wa Hotel ya Lamada Ilala Dar, nyota hao waliofanya kweli kwenye muvi ya ‘Da er Salaaam Sister’ walianika kuwa miezi mitano iliyopita walianza kuwasiliana na dairekta huyo, ikiwa ni pamoja na kumtumia moja ya kazi zao, na sasa mambo yameshaiva kwani amewaita na tayari washakamilisha taratibu za kupata pasi za kusafiria.

“tuko tayari kwa safari ya kwenda kufanya kazi Nollywood mapema mwezi ujao, hizi unazoziona hapa ndiyo pasi zetu za kusafiria”, alisema Shilole huku akionyesha ‘Passport’ yake.

Posted by Dismas Ten in | Thursday, December 23, 2010 1 comment
Shilole akiwa 'bize' na kutafuna Kiti Moto's
PAMOJA na kuwa ni muumini wa dini ya Kiislamu, nyota kutoka kiwanda cha filamu Bongo Zuwena Mohamed ‘Shilole’ juzikati alinaswa akibugia ‘Kiti moto’ (nyama ya nguruwe) mchana kweupe bila wasiwasi wowote. Tukio la nyota huyo kunaswa akila nyama hiyo iliyopewa alama X katika vitabu vya Mwenyezi Mungu, lilitokea Jumatano ya wiki hii katika Baa maarufu ya Panama iliyopo maeneo ya Kinondoni Studio jijini Dar es Salaam.
Dakika chache baada ya kumaliza ‘kufakamia’ haramu hiyo Shilole alifunguka kuwa hafahamu lolote kama kula Kiti Moto ni haramu kwani tangu ameanza kula nyama hiyo hajawahi kuvimba miguu wala kushindwa kutembea kwa hiyo anahisi hana kosa lolote kula kile ambacho moyo wake unapenda. “Kila mtu anao huru wa kufanya kile anacho kipenda sharti tu asivunje sheria za nchi na katika sheria za Bongo hakuna sehemu iliyoandikwa Watanzania marufuku kula Kiti moto ndiyo maana mimi na kula kwa sababu naizimia sana na sijawahi kupata tatizo lolote toka nimeanza kutafuna nyama hii ” alisema Shilole. Katika hatu nyingine nyota huyo wa filamu ya ‘Dar es Salaam Sister’ alienda mbali zaidi na kusema katika ulimwengu huu si watu wote watakaouona Ufalme wa Mungu, na kama kula Kiti Moto ni dhambi kubwa basi duniani hakuna atakaye pona kwani hata hao wanaojiita wenye dini nao wana kula nyama hiyo. “Kuna watu hapa duniani wanafanya mambo ya ajabu kuliko hata hili la mimi kula Kiti Moto lakini hayasemwi na kama kula nyama hii ndiyo zambi kubwa basi hakuna atakayepona, hebu jiulize na wewe kiongozi wa dini aliyeoa shoga ama kiongozi fulani anayechukua mke wa mtu na mimi ninayekula Kiti Moto nani ananafuu ? alimaliza Shilole kwa kwa kuhoji.



TAFUTA HAPA

UNGANA NASI

Delicious Digg Facebook Favorites More Stumbleupon Twitter